
Msanii wa muziki wa asili kutoka Kanda ya Ziwa, Mjukuu wa Mwanamalonde maarufu Mwamba wa Kanda ya Ziwa au Ngonho ameachia wimbo mpya unaoitwa “Mbiti Yane - Fisi Wangu” ambao umeanza kufanya vizuri kwa mashabiki wa muziki wa asili na utamaduni. Wimbo huo umewekwa rasmi kwenye mtandao wa YouTube ukiwa na mahadhi ya asili yenye ujumbe wa kijamii pamoja na vionjo vya utamaduni wa Kisukuma vinavyoendelea kumtofautisha msanii huyo.
Katika wimbo huo mpya, Mjukuu wa Mwanamalonde anaonesha ubunifu wa kipekee kupitia uimbaji, mavazi ya asili pamoja na matumizi ya lugha na methali za kijadi zinazobeba mafunzo kwa jamii.
Social Plugin