
Gari la Msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga limepata ajali eneo la Usanda wilaya ya Shinyanga barabara ya Tabora - Shinyanga, wakati likikwepa gari aina ya Toyota Harrier na kuingia kwenye mtaro.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa watu watano wamejeruhiwa katika ajali hiyo akiwemo Mwandishi wa Habari wa ITV/Radio One Bw. Frank Mshana, Johnson Zacharia na Boazi.
Majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga.
Taarifa zaidi zitawajia kadiri tutakavyo zipata.
CHANZO - ITV
Social Plugin