Picha : MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA MKUTANO MKUU WA CCM LEO DODOMA

Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. John Magufuli akifungua Mkutano Mkuu wa tisa wa CCM, katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, Dodoma, leo. Pamoja na mambo mengine kuhusu mageuzi ndani ya Chama, uadilifu na usimamizi wa mali za Chama ili Chama kisitegemee wafadhili wakiwemo matajiri wachache, amemtaka Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana kuendelea kumsaidia katika nafasi hiyo ya Katibu Mkuu katika kipindi kingine cha miaka mitano
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimsalimia Balozi wa China hapa nchini Wang Ke, alipokuwa akisalimia mabalozi kutoka nchi mbalimbali ambao wamehudhuria Mkutano huo 
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo wakikagua mazingira ya nje ya ukumbi kabla ya mkutano huo mkuu kuanza
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akiandaa mazingira ya kuchangamsha ukumbi kabla ya mkutano huo kuanza. Kushoto ni katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga
Wanakwaya wa TOT wakiimba wimbo maalum wa kumkaribisha ukumbini Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk John Magufuli
Wajumbe wakijimwayamwaya ukumbini kushangilia wakati Mwenyekiti wa CCM Taifa, akiingia ukumbini
Mwimbaji wa TOT akiimba wimbo wa kuhamasisha mapokezi ya Mwenyekiti ukumbini
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Jakaya Kikwete na Mwenyekiti mstaafu wa CCM Ali Hassan Mwinyi wakimsubiri Mwenyekiti Kuingia Ukumbini. Mzee Mwinyi akisoma toleo maalum la gazeti la Uhuru wakati akisubiri
Viongozi waliotangulia meza kuu wakisimama kumlaki Mwenyekiti wa CCM rais Dk John Magufuli wakati akiingia ukumbini
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli akisalimia viongozi mbalimbali baada ya kuingia ukumbini. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli akiwa tayari ukumbini. Wengine kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mstaafu Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa CCM Rais wa Zanzibar Dk. Shein, Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, Makamu Mwenyekiti wa CCM-bara Philip Mangula na Mwenyekiti Mstaaafu wa CCM Benjamin Mkapa
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Maguduli akijadili jambo na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana baada ya kuketi ukumbini
Waimbaji wa TOT wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya Mkutano kuanza
Wajumbe wakiwa wamesimama kuimba wimbo wa Taifa
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk John Magufuli na viongozi wengine meza kuu wakiimba wimbo wa Taifa huku wamesimama kwa ukakamavu 
Viongozi wakiwa wameketi baada ya kuimba wimbo wa taifa
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiondoka meza kuu kwa ukakamavu kwenda kufuatilia jambo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti kufungua Mkutano huo
Wapiga picha wakifuatilia matukio
Mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere Mama Maria Nyerere akiwa na Mama Salma Kikwete kwenye mkutano huo
Baadhi ya wageni waalikwa na wajumbea wakiwa kwenye mkutano huo
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli (kulia)akifungua mkutano huo mkuu
Wajumbe wakishangilia baada ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli kumtaka Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kuendelea kumsaidia katika nafasi hiyo ya Ukatibu Mkuu kwa miaka mingine mitano
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akionekana kutafakari baada ya kauli ya Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli kumhitaji tena
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiinuka kuonyesha ishara ya kukubali makakwa ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. Magufuli. Kulia ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Zanzibar Dk Amani Abeid Karume na Mzee Mkapa ambaye anacheka kuonyesha kuunga mkono
Baadhi ya waliohamia CCM kutoka vyama vya upinzani wakisimama baada ya kutmbulishwa na Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli kwenye mkutano huo
Mwenyekiti wa CCM Rais Dk Magufuli akipongezwa na Mwenyekiti mstaafu wa CCM Jakaya Kikwete baada ya hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Bara Pius Msekwa 
"Hotuba imeshiba" inaelekea ndivyo Kikwete alivyomwambia Dk Magufuli baada ya kumpongeza 
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimpongeza Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli baada ya hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo
Dk Magufuli akipongezwa na Makamu Mweenyekiti wa CCM Bara Philip Mangula kwa hotuba nzuri ya ufunguzi wa mkutano huo
Dk. Magufuli akipongezwa na Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Zanzibar Amani Karume baada ya hotuba
Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli akirudi katika nafasi yake baada ya kutoa hotuba na kufungua mkutano huo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akitoa maelezo kuhusu CCM ilivyotekeleza kazi zake katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. kabla ya hapo alitumia fursa hiyo kumshukuru Mwenyekiti wa CCM Dk Magufuli kwa kumwamini tena ili aendelee kumsaidia. Kinana amemwahidi kumsaidia kwa weledi na uaminifu mkubwa
TOT wakimshangilia Mwenyekiti Dk. Magufuli baada ya hotuba yake

KABLA YA MKUTANO
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimpokea Makamu Mwenyekiti wa CCM Rais wa zanzibar Dk Ali Mohammed Shein alipowasili kwenye mkutano huo
Dk Shein akimsalimia Mzee Mkapa
Dk Shein akimsalimia Mzee Karume. Katikati ni Kikwete
Dk Magufuli akiongozana na Dk Shein, Mzee Mangula na Ndugu Kinana kwenda ukumbini
Kabla ya mkutano kuanza, baadhi ya wajumbe wakiperuzi nakala za toleo maalum la gazeti la Uhuru kuhusu mkutano huo
Wajumbe wakipozi picha ya kumbukumbi ukumbini
Baadhi ya wafanyakazi waandamizi wa Uhuru Publications Ltd, wachapichaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani wakiwa ukumbini
Mwanadiplomasia akisoma gazeti la Uhuru
Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa CCM Bara John Chiligati akisoma toleo maalum la gazeti la Uhuru
Katibu Mwenezi wa CCM Humphrey Polepole akijadili jambo na Afisa Mwandamizi wa CCM Frank Uhahula. kulia ni Kanali Mstaafu Ngemela
Maofisa wa CCM wakiwa ukumbini kusimamia masuala ya Itifaki
Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Yusuf Makamba akisalimiana na Mzee John Butiku
Vijana Jazz wakirindima ukumbini
Baadhi ya watangazaji wa UHURU FM wakiwa nje ya ukumbi kurusha live matangazo ya mkutano huo mkuu
Baadhi ya wageni waalikwa wakisalimiana ukumbini
Mama Janeth Magufuli akiwasili ukumbini
Wajumbe ukumbini
Wajumbe ukumbini
Wapigapicha Muhidin Issa Michuzi aka Ankal na Adam Mzee wakicheki mazingira ukumbini
Wafanyakazi wa Makao Makuu ya CCM, Lumumba wakiwa ukumbini
Wasanii wa TOT wakipumzika ukumbini baada ya awamu ya kwanza ya kutumbuiza kumalizika. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527