Ushirikina Mwanza!! MTI WAONGEA KAMA BINADAMU UKIGOMA KUNG'OLEWA KUPANUA BARABARA...TAZAMA VIDEO HAPA


Wakazi wa Barabara ya Iloganzala Jijini Mwanza jana walipigwa butwaa baada ya mti aina ya mwembe kutoa sauti kama binadamu ukipinga using'olewe. 


Tukio hilo limetafsiriwa kuwa la kishirikina ama mazingaombwe ikizingatiwa kwamba si jambo lenye uhalisia mti kuongea kama binadamu. 


Katika eneo la Iloganzala Jijini Mwanza kuna upanuzi wa barabara inayoelekea Uwanja wa ndege wa Mwanza. 

Shughuli ya kuung'oa mti huo aina ya mwembe leo imeendelea ikiwa ni siku ya pili ya kukabiliana na mwembe huo na hatimaye wamefanikiwa kuung'oa huku mamia ya wananchi wakishuhudia tukio hilo la ajabu.

Kwa mujibu wa maelezo kutoka wananchi wa eneo hilo wanasema jirani na mti huo kuna nyumba iliwahi iligoma kubomolewa wakati wa upanuzi wa barabara

Tazama Video hapa chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527