MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AJIUZULU..PIA KUNA MAJAJI WAWILI...RAIS MAGUFULI ARIDHIA

Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli ameridhia maombi ya kuacha kazi kwa viongozi wafuatao;


1. Ndg. Saidi Meck Sadiki - Aliyekuwa mkuu Wa Mkoa wa Kilimanjaro.


2. Ndg. Aloysius Kibuuka Mujulizi - Aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.


3. Ndg. Upendo Hillary Msuya - Aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania.


Taarifa iliyotolewa leo tarehe 16 Mei, 2017 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi inaeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli ameridhia maombi ya kuacha kazi kwa viongozi hao kuanzia tarehe 15 Mei, 2017.


Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais,
IKULU Dar es Salaam 
16 Mei, 2017

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527