MGOMBEA UBUNGE WA CCM AOMBA RADHI KUIGARAGAZA VIBAYA CCM AKIWA CUF

Mgombea ubunge jimbo la Kinondoni (CCM), Maulid Mtulia amewaomba radhi wanachama wa chama hicho tawala kwa ushindi wa kishindo alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 akiwa CUF.

Mtulia ametoa kauli hiyo leo Januari 21, mwaka 2018 wakati akitambulishwa kwa wanachama wa chama hicho wilaya ya Kinondoni.

Mwaka 2015, Mtulia alishinda ubunge wa Kinondoni kwa tiketi ya CUF, lakini Desemba 2 mwaka jana alijivua uanachama wa chama hicho na kuhamia CCM, hivyo kupoteza sifa ya ubunge. 

Hata hivyo CCM kilimpitisha kugombea ubunge katika jimbo hilo.

Na Jackline Masinde na Pamela Chilongola,Mwanachi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527