KESI YA VIGOGO WA SIMBA YAPIGWA KALENDA HADI SEPTEMBA 8,2017

Upande wa Mashtaka katika kesi inayomkabili Rais wa Simba, Evans Aveva na Makamu wake Geofrey Nyange ‘Kaburu’ leo umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa wamekusanya nyaraka za upelelezi na zimepelekwa kwa mtaalamu wa maandishi.


Hayo yamesemwa na Wakili wa Serikali, Estazia Willson mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa wakati kesi hiyo ilipoitishwa kwa ajili ya kutajwa.


Wakili Wilson amedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, pia wamekusanya nyaraka na zimepelekwa kwa mtaalam wa maandishi, hivyo wanasubiri ripoti.


Hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi September 8, 2017.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527