BASI LA WIBONELA LA DAR - KAHAMA LIMEGONGANA NA BASI LA TAKBIIR KIBAIGWA

Habari tulizozipata hivi punde ni kwamba basi la Wibonela Express lenye namba za usajili T158 CEX lililokuwa linatoka Dar es salaam kuelekea Kahama mkoani Shinyanga limegongana na basi la Tak-biir lenye namba za usajili T818 CYQ katika eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma ambapo ujenzi wa barabara unaendelea.


Taarifa zinasema hakuna abiria aliyepoteza maisha lakini watu kadhaa wamejeruhiwa.

Baadhi ya abiria waliokuwa kwenye basi la Wibonela wanasema chanzo cha ajali hiyo ni dereva wao ambaye alikuwa anaendesha basi kwa mwendo kasi na hakujali malalamiko ya abiria wake kila walipomwambia apunguze mwendo.

"Hii ni mara ya pili,ya kwanza tulinusurika kupata ajali,alikuwa anaovatek 'anajaribu kuyapita magari mengini' bila  kuchukua tahadhari,ukiwaambia wanakuwa wabishi",wamesema.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments