News Alert !! WACHEZAJI WA RUVU SHOOTING WAPATA AJALI SINGIDA

Gari lililobeba wachezaji wa Ruvu Shooting likiwa limepata ajali


Habari tulizozipata hivi punde ni  kwamba msafara wa timu ya Ruvu Shooting umepata ajali mbele kidogo ya Singida wakiwa safarini kurejea Dar es salaam.

Taarifa kutoka kwa mmoja wachezaji waliokuwapo inasema kwamba gari likiwa katika mwendo tairi lilipasuka na kusababisha gari kuhama njia na kuparamia miti iliyokuwa jirani.

Hakuna mtu yoyote aliyeumia sana japo kuna mchezaji mmoja ambaye amepata majeraha ya kawaida.
Taarifa zaidi tutawaletea hivi punde....

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527