WAANDISHI WA HABARI 10 WAKAMATWA NA POLISI ARUSHA, MEYA WA JIJI NAYE YUPO CHINI YA ULINZI


NB-picha kutoka maktaba siyo ya waandishi waliokamatwa



Habari zilizotufikia hivi punde kutoka mkoani Arusha ni kwamba waandishi wa habari 9 wamekamatwa na polisi wakati wakitekeleza majukumu yao.


 Inaelezwa kuwa waandishi wamekamatwa na jeshi la polisi Arusha kwa madai ya kuhudhuria kikao ambacho hakikuwa na kibali katika shule ya Lucky Vincent ambapo shirikisho la wamiliki wa shule binafsi walikuwa wanaenda kutoa rambirambi lakini baada ya kupata taarifa walienda kufanya kazi ndipo wakaambulia kukamatwa na polisi
Inaelezwa kuwa mbali na waandishi wa habari kukamatwa pia Meya wa Jiji la Arusha Mstahiki Kalisti Lazaro, Wamiliki wa shule, Viongozi wa dini nao wamekamatwa katika eneo la shule ya Lucky Vicent Arusha walipokuwa wamekwenda kutoa rambirambi.

Waandishi wa habari waliokamatwa na polisi
1 .Godfrey Thomas -Ayo Tv

2.Alphonce Saul Kusaga- Triple  A

3.Filbert Rweyemamu- Mwananchi

4.Hussein Tuta Itv

5.Joseph Ngilisho-Sunrise radio

6.Geofrey Stephen- Radio 5

7.Janeth Mushi -Mtanzania

8.Zephania Ubwani- The Citizen

9.Elihuruma Yohani- Tanzania Daima

10.Idd Uwesu -Azam Tv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527