RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MWINGINE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Geoffrey Idelphonce Mwambe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).


Kabla ya Uteuzi huo Bw. Geoffrey Idelphonce Mwambe alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida.


Nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Manyoni itajazwa baadaye.


Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Clifford Tandari kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro.


Bw. Clifford Tandari anachukua nafasi ya Dkt. John Ndunguru ambaye amestaafu.


Kabla ya uteuzi huo Bw. Clifford Tandari alikuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).


Uteuzi wa viongozi hao unaanza mara moja.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527