RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MWINGINE,KAGUSA BENKI KUU YA TANZANIA (BOT)



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 31 Mei, 2017 amefanya uteuzi wa Naibu Magavana wawili wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT).


Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Yamungu Kayandabila kuwa Naibu Gavana anayeshughulikia Uchumi na Fedha (Economic and Financial Policies – EFP).


Kabla ya uteuzi huu Dkt. Yamungu Kayandabila alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazina anachukua nafasi iliyoachwa na Dkt. Natu E. Mwamba ambaye amemaliza muda wake.


Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Bernard Yohana Kibese kuwa Naibu Gavana anayeshughulikia Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha (Financial Stability and Deepening – FSD).


Kabla ya Uteuzi huo Dkt. Bernard Yohana Kibese alikuwa ni Mtaalamu wa Uchumi na Fedha wa BOT na anachukua nafasi iliyoachwa na Lila H. Mkila ambaye amemaliza muda wake.


Uteuzi huu unaanza mara moja.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
31 Mei, 2017

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments