
Kamanda Justus Kamugisha
Mtoto aitwaye Happiness Kashindye mwenye umri wa miaka 9 mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya msingi Negezi iliyopo kata ya Ndala Manispaa ya Shinyanga ameuawa kikatili kwa kubakwa
kisha kutobolewa macho na watu wasiofahamika kisha mwili wake kutupwa kichakani.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea jana saa saba mchana katika kitongoji cha Kashampa kijiji cha Nhelegani
kata ya Kizumbi ambapo mwili wa marehemu ulikutwa kichakani.
Kaimu mganga mfawidhi wa
hospitali ya Mkoa wa Shinyanga Dkt Daniel Maguja amesema vipimo vinaonesha kuwa mtoto huyo alibakwa na kutobolewa macho.
Kamanda wa polisi mkoani hapa Justus Kamugisha amethibitisha kutokea kwa tukio
hilo na kuongeza kuwa chanzo cha tukio
hilo kinachunguzwa huku akitoa wito kwa wananchi kutoa taarifa zitakazosaidia kuwabaini na kuwakamata wauaji ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Na Kadama Malunde-Shinyanga
TAFADHALI BOFYA HAPA U LIKE PAGE YETU TUKUTUMIE "HABARI" MOJA KWA MOJA KILA ZINAPOTOKEA
TAFADHALI BOFYA HAPA U LIKE PAGE YETU TUKUTUMIE "HABARI" MOJA KWA MOJA KILA ZINAPOTOKEA
Social Plugin