Sakata la usajili wa mchezaji wa kiargentina Angel Di Maria kwenda klabu ya Manchester United kutoka Real Madrid limemalizika rasmi leo hii.
Manchester United wamethibitisha kukamilisha usajili wa Di Maria kutoka Real kwa ada ya uhamisho £59.7m ambayo imeweka rekodi mpya ya uhamisho nchini Uingereza – ikivunja rekodi ya £50m ambayo Chelsea waliilipa Liverpool kwa ajili ya usajili wa Fernando Torres.
Di Maria amekabidhiwa jezi namba 7 na amesaini mkataba wa miaka mitano wa kuitumikia Manchester United.





Social Plugin