Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

TRA SHINYANGA YAZINDUA OFISI INAYOTEMBEA, YAWAFUATA WALIPAKODI MNADA WA TINDE KUWAPELEKEA HUDUMA KARIBU

    

Ofisi inayotembea ya Mamlaka ya mapato Tanzania TRA  kusogeza huduma karibu na wananchi na kupunguza changamoto ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma 
                           Semeni Mbeshi Afisa wa kodi wa TRA akizungumza wakati wa kutoa elimu kwa wananchi juu ya masuala ya kodi katika mnada wa Tinde ikiwa ni hatua ya kusogeza huduma karibu kwa wananchi kupitia ofisi inayotembea.

Na Malunde 1 Blog

 Katika jitihada za kusogeza huduma karibu kwa wananchi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Shinyanga imeanza rasmi kutoa huduma kupitia ofisi inayotembea, hatua inayolenga kupunguza changamoto ya walipakodi kusafiri umbali mrefu kufuata huduma .

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo katika mnada wa Tinde Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga leo Juni 16,2026  Afisa wa Kodi wa TRA Mkoa wa Shinyanga Semeni Mbeshi amesema ofisi inayotembea imeanza rasmi kutoa huduma katika eneo hilo ikiwa ni sehemu ya mkakati wa TRA wa kuwafikia walipakodi moja kwa moja katika maeneo yao ya biashara.

Amesema huduma hiyo itawawezesha wananchi kupata huduma mbalimbali za kikodi kwa urahisi, kupunguza gharama na muda wa kufuata huduma katika ofisi za TRA pamoja na kutoa fursa ya kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati.

Kupitia ofisi inayotembea wananchi wamepatiwa huduma zote zinazotolewa na TRA huku akitoa rai kwa wengine kuchangamkia fursa hiyo .

 Baadhi ya wafanyabiashara waliohudumiwa katika mnada wa Tinde wameipongeza TRA kwa kuanzisha huduma hiyo, wamesema imewarahisishia upatikanaji wa huduma na kuwapunguzia usumbufu wa kusafiri umbali mrefu.

Wameiomba TRA kuendelea kupeleka huduma ya ofisi inayotembea katika maeneo mengine ili walipakodi wengi zaidi wanufaike na huduma hiyo, wakieleza kuwa hatua hiyo itachangia kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma na kuimarisha ushirikiano kati ya mamlaka hiyo na wananchi.

TRA inaendelea kutoa huduma katika maeneo mbalimbali kupitia ofisi inayotembea na kuwaomba kuchangamkia fursa hiyo.

Wananchi wakipatiwa huduma kupitia ofisi inayotembea ya TRA
            
           
    

Semeni Mbeshi Afisa wa kodi wa TRA akizungumza wakati wa kutoa elimu kwa wananchi juu ya masuala ya kodi katika mnada wa Tinde ikiwa ni hatua ya kusogeza huduma karibu kwa wananchi kupitia ofisi inayotembea.

                      
        
            
            
        
          
       

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com