Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MISA TANZANIA YAHUDHURIA UWASILISHAJI WA BAJETI YA WIZARA YA HABARI BUNGENI DODOMA

Na Mwandishi wetu - Dodoma

Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA Tanzania), leo imehudhuria kikao cha Bunge Jijini Dodoma kilichohusisha uwasilishaji wa mapendekezo ya bajeti ya Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

MISA Tanzania ilikuwa miongoni mwa taasisi za kihabari zilizoshiriki katika uwasilishaji huo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za wadau wa sekta ya habari kufuatilia na kushiriki michakato ya maamuzi yenye athari kwa maendeleo ya tasnia hiyo nchini.

Taasisi hiyo iliwakilishwa na Mwenyekiti wake, Edwin Soko, ambaye alihudhuria kikao hicho kwa lengo la kufuatilia kwa karibu vipaumbele vya wizara hiyo, hususan katika maeneo yanayohusu uhuru wa vyombo vya habari, maendeleo ya wanahabari, na mazingira wezeshi ya utendaji kazi wa sekta ya habari.

Ushiriki wa MISA Tanzania katika kikao hicho unaakisi dhamira ya taasisi hiyo katika kuhakikisha uwajibikaji, uwazi, na ushirikishwaji wa wadau katika masuala muhimu yanayogusa sekta ya habari nchini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com