Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MAHAFALI YA KWANZA YA “WANAWAKE NA SAMIA” CHUO CHA UFUNDI STADI - VETA SHINYANGA


Na Mwandishi Wetu.

Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga kinafanya mahafali ya kwanza kwa wahitimu wa programu maalum ya Wanawake na Samia, ambapo jumla ya wanawake 81 wanahitimu mafunzo ya ufundi bure katika fani mbalimbali.

Mahafali hayo yamefanyika leo Oktoba 2, 2025, yakihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, ambaye amempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha programu hiyo inayowawezesha wanawake kupata ujuzi wa ufundi na kujikwamua kiuchumi.

“Mafunzo haya yanawajengea uwezo wa kujiajiri na kuimarisha uchumi wa familia zenu, hivyo natoa rai kwa wahitimu kuunda vikundi vya ujasiriamali ili wanufaike na mikopo isiyo na riba inayotolewa na Halmashauri kwa asilimia 10, ambapo wanawake wananufaika kwa asilimia nne. Pia anawasihi kutumia fursa za mikopo na miradi inayotolewa na taasisi mbalimbali za kifedha”, amesema Mhita.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Samia Taifa, Futuma Madidi, amemshukuru Rais Samia kwa kuanzisha programu hiyo, huku akiomba serikali iwape wahitimu vipaumbele katika zabuni na fursa nyingine za kiuchumi.

Mkuu wa Chuo cha VETA Shinyanga, Abraham Mbughuni, amebainisha kuwa wahitimu hao wamesoma fani mbalimbali ikiwamo ushonaji (26), saluni (25), umeme (10), bomba (7), udereva (4), mapambo (4), mapishi (3) na kompyuta (2).

Baadhi ya wahitimu akiwamo Zainabu Joseph wanamshukuru Rais Samia kwa kuwapatia nafasi ya kujifunza bure, wakisema ujuzi huo unawasaidia kuendesha maisha na kujipatia kipato.

<<<TAZAMA  PICHA MATUKIO MBALIMBALI>>>

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Samia Taifa, Futuma Madidi akizungumza kwenye mahafali hayo.
Mkuu wa Chuo cha VETA Shinyanga, Abraham Mbughuni akizungumza kwenye mahafali hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita akizungumza kwenye mahafali hayo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com