Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MGOMBEA UBUNGE AZZA HILLAL HAMAD ANAZINDUA KAMPENI JIMBO LA ITWANGI


Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa Jimbo jipya la Itwangi, Azza Hillal Hamad, leo Septemba 13, 2025 anazindua rasmi kampeni zake katika Mkutano mkubwa wa hadhara unaofanyika Didia, wilayani Shinyanga.

CCM inaendelea kuwaomba wananchi wa Jimbo la Itwangi kumpa kura za ushindi ili awe mwakilishi wao bungeni.

Vilevile, inasisitiza umuhimu wa wananchi wote kujitokeza kwa wingi kumpigia kura Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, mgombea urais kupitia CCM pamoja na Madiwani wa CCM.

Mkutano huu ni sehemu ya maandalizi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, ambapo wananchi watapiga kura kuwachagua viongozi wa ngazi mbalimbali.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com