Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka wadau wa usafirishaji kuendelea kushirikiana na Jeshi hilo na kutoa mchango wao utakao saidia kupunguza ajali zinazosababisha vifo na majeruhi kwa watumiaji wa vyombo vya usafiri.
IGP Sirro amesema hayo leo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji nchini katika kikao kazi cha kufanya tathimini, changamoto na mafanikio kwa kipindi cha mwaka mzima.
Aidha, IGP Sirro ametoa maagizo kwa Makamanda wa Polisi nchini kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa magari katika maeneo yaliyoainishwa na kuepuka kusimamisha magari mara kwa mara.
Naye mdau wa usafirisha bwana Enos Lema, ameiomba serikali pamoja na mamlaka zinazohusika kuangalia upya suala la mabasi ya abiria yanayofanya safari zake mikoani pamoja na nchi jirani kuruhusiwa kuanza safari hata nyakati za mchana hatua itakayowezesha kupunguza changamoto za usafirishaji kwa abiria.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin