MWIMBAJI WA INJILI KUTOKA KENYA ANAYEDAIWA KUPEWA UJAUZITO NA HARMONIZE AFUNGUKA

Siku mbili hizi kuna stori zilienea Kwenye mitandao ya kijamii zilizosema kuwa Msanii wa Bongo fleva kutoka WCB Harmonize amempachika mimba mwanadada ambaye ni msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya.


Msanii huyo anayejulikana kama Veronica Wanja ‘Nicah The Queen’ amekataa tuhuma hizo na kudai kuwa hazina ukweli wowote, awali Nicah alikuwa katika mahusiano na mchekeshaji Dr. Ofweneke’s.


Tetesi hizi zimekuja mara baada ya wasanii hawa kuonekana pamoja mara kwa mara hali iliyozua minong’ono.


Kwenye Interview aliyofanya na gazeti moja nchini humo Veronica alisisitiza kuwa yeye sio mjamzito na hapendi kuongelea sana hayo mambo kwa sababu yeye ni Msanii wa injili hivyo si vema kuongelea.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527