MSAKO MKALI KUFANYIKA KUKAMATA OMBA OMBA WA BARABARANI

Mamlaka katika mji mkuu wa Rwanda, Kigali imetangaza kuanza msako mkali na kuwaweka gerezani walemavu wote wanaojihusisha na vitendo vya kuomba omba barabarani, kwa madai kuwa ni chanzo cha uchafu wa jiji hilo.

Msako huo unaweza kutekelezwa wakati wowote kuanzia sasa, umewaonya walemavu hao kuwa kama hawataacha kuomba omba watakabiliwa na kifungo.

Baadhi ya wananchi wamepinga uamuzi huo wakisema, unalenga kukandamiza walemavu na watu masikini ambapo mashirika ya kiraia nchini Rwanda yameshauri kwamba kabla ya utekelezaji wa msako huo yafanyike mazungumzo ya pande zote. 

Ripoti mbalimbali zimekuwa zikiitaja Kigali kuwa miongoni mwa majiji masafi barani Afrika huku ripoti nyingine hususani zile za kutetea haki za binadamu, zikiishutumu serikali kwa kuwafunga watu wasiojiweza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527