KIKWETE AMMWAGIA BARAKA ALI KIBA BAADA YA KUMTEMBELEA NA KUMPA TAARIFA YA KUOA MWEZI HUU

Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amefunguka na kumshukuru msanii Alikiba kwa kumtembelea nyumbani kwake leo na kusema kuwa amempa taarifa kuwa ataoa hivi karibuni.


Kikwete amesema hayo leo April 14, 2018 kupitia mtandao wake wa twitter na kusema kuwa msanii huyo ambaye sasa bado anafanya vyema na wimbo wake wa 'Seduce me' amemwambia anatarajia kuoa siku za karibuni.


"Namshukuru Alikiba kuja kunitembelea na kunitaarifu kuwa anatarajia kuoa hivi karibuni. Nimempatia nasaha zangu na kumtakia kila la kheri kwa jambo hilo jema aliloamua kufanya"alisema Kikwete 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527