HAYA HAPA MAAMUZI YA BASATA VIDEO YA NANDY,BILL NAS UCHI MTANDAONI

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limefunguka na kuweka wazi kuwa siku ya jana April 13, 2018 lilikutana na msanii Nandy kufuatia kuvuja kwa video yake akiwa faragha na msanii Bill Nas na kufanya naye mazungumzo.


BASATA wameweka wazi kuwa katika mkutano hao ambao ulifanyika jana wamemtaka msanii huyo kwanza kuomba radhi Watanzania kwa kitendo hicho lakini pia baraza hilo limechukua jukumu la kuwakumbusha wasanii wengine juu ya matumizi ya mitandao ya kijamii na kuwataka kutumia mitandao ya jamii kwa lengo la kujiletea maendeleo. 

"Baraza linawakumbusha na kuwaasa wasanii wote kutumia maendeleo ya teknolojia na mitandao ya kijamii kwa lengo la kujiletea maendeleo badala ya kutumia mitandao kusambaza vitu visivyo na manufaa kwao na vyenye kuwadhalilisha wao wenyewe, familia zao na umma kwa ujumla" alisema taarifa ya BASATA 

Hata hivyo msanii Nandy jana alipotoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) aliweza kuandika maelezo marefu na kuomba radhi kwa Watanzania kwa kitendo cha video yake ya faragha kuvuja mtandaoni. 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527