KAIMU KATIBU WA IDARA YA VYUO NA VYUO VIKUU NDUGU ZENDA AKABIDHI KADI 1500 KWA KATIBU HAMASA SENETI YA DAR


Kaimu Katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu Ndugu Daniel Zenda akikabidhi kadi 1500 za wanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kwa Katibu wa Hamasa Seneti ya mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Juakali Kuwanya katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya UVCCM, Upanga jijini Dar es Salaam.

Zenda amesema, kadi hizo amezikabidhi ili zigawiwe kwa wananchama wapya ambao wamekuwa wakijiunga kwa wingi katika Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake, kutokana na mwamko mkubwa wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuunga mkono CCM kutokana na kuvutiwa na Utendaji kazi wa Rais John Magufuli na Serikali yake ya awamu ya tano

Imetolewa na  Uvccm Seneti Mkoa Dar es salaam

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527