DIWANI WA CHADEMA AJIUZULU NA KUJIUNGA CCM




Diwani wa Hayderer (Chadema) wilayani Mbulu mkoani Manyara, Justin Masuja amejiuzulu nafasi hiyo na kujiunga na CCM.

Masuja amejiunga na CCM leo Februari 12,2018 katika ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti.

Katika mkutano wa hadhara, Mnyeti aliwataka madiwani wa upinzani kuhamia chama tawala ili watekeleze ilani ya CCM ambayo ndiyo ipo madarakani.

Diwani huyo amesema anajiunga na CCM ikiwa ni hatua ya kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli katika kuwatumikia wananchi.

Na Joseph Lyimo, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527