TIGO YAWATUNUKU ZAWADI KWA MAWAKALA WAKE WA TIGO PESA KANDA YA ZIWA NA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI


Mwakilishi wa mshindi wa Tigo pesa wakala David Lucas,Joyce David(wa pili kushoto) akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Joseph Mutalemwa(kulia), wakati wa hafla ya kuwapa zawadi mawakala waliofanya vizuri kwenye miamala ya Tigo pesa iliyofanyika jijini Mwanza jana, kushoto ni Mratibu wa Tigo wa Masoko na Biashara kanda ya Ziwa Abraham Mchau akishuhudia.
Mwakilishi wa mshindi wa Tigo pesa wakala kutoka Kahama mkoani Shinyanga Asha Athuman,Daud Kilonzo akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Joseph Mutalemwa(kushoto), wakati wa hafla ya kuwapa zawadi mawakala waliofanya vizuri kwenye miamala ya Tigo pesa iliyofanyika jijini Mwanza jana, kulia ni Meneja wa Tigo kanda ya Ziwa Kaskazini Daniel Mainoya akishuhudia.
Washindi wa Tigo pesa wakionyesha mfano wa hundi zao baada ya kukabidhiwa jijini Mwanza. 
Mawakala na wateja wa mtandao wa Tigo wakishundua utoaji wa hundi kwa wateja wa tigo pesa jijini Mwanza. 
Mawakala na wateja wa mtandao wa Tigo wakishundua utoaji wa hundi kwa wateja wa tigo pesa jijini Mwanza. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Tigo-Tanzania Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jackson Kiswaga (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi ya Sh1 milioni Wakala wa Tigo Pesa, Asha Ramadhani kutoka Mkoani Ruvuma baada ya kuibuka mshindi kwa kufanya vizuri kwenye huduma ya TigoPesa katika droo inayochezeshwa na kampuni hiyo. Hafla hiyo ilifanyikia Makao Makuu ya Ofisi za Tigo Kanda hiyo zilizopo Uhindini Jijini Mbeya.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Tigo-Tanzania Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Jackson Kiswaga (kutikati) akizungumzia zawadi zilizotolewa kwa washindi wa droo inayochezeshwa kwa mawakala wa Tigo Pesa, Yusuph Kigomba (kushoto) kutoka Mkoani Iringa na Asha Ramadhani kutoka mkoani Ruvuma ambao waliibuka washindi kwa kufanya vizuri kwenye huduma ya TigoPesa. Hafla hiyo ilifanyikia Makao Makuu ya Ofisi za Tigo Kanda hiyo zilizopo Uhindini Jijini Mbeya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527