Picha : YALIYOJIRI KWENYE SHEREHE YA HARUSI YA SHILOLE


Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva na Mjasiriamali, Shilole ‘Shishi Baby” jana amefanya sherehe ya harusi yake aliyofunga na mumewe Uchebe katika ukumbi ulioko Mikocheni, jijini Dar es Salaam.


Sherehe hiyo ilipambwa na burudani mbalimbali na ilihudhuriwa na mastaa mbalimbali wa filamu na muziki wa Bongo Fleva.


Wasanii mbalimbali waliohudhuria katika sherehe hizo walijaribu kumfurahisha bibi harusi pamoja na mumewe kwa staili tofauti tofauti huku zikiambatana na zawadi kem kem.


Rais wa WCB, Diamond Platnumz alitoa kali ya mwaka katika sherehe ya harusi ya Shilole na Uchebe baada ya kumtaka bibi harusi huyo kuchagua zawadi ambayo anaitaka kutoka kwake. Baada ya Diamond kusema hivyo, Shishi alimuomba Diamondi kumsaidia kuitangaza biashara yake mpya ya Shishi Chili, ambapo Diamond alikubali ombi hilo.


Naye msanii ambaye yuko chini ya lebo ya WCB, Harmonise hakuacha kuonyesha makali yake baada ya kumtaka Shilole atafute gari aina ya Toyota Noah, yenye thamani ya shilingi za kitanzania, milioni 9 ambayo yeye (Harmonise) atailipia na itatumika katika kurahisisha biashara za Shishi.


Kwa upande wao Jux na Vanessa nao hawakubaki nyuma, ambapo Jux aliahidi kumlipiaa ada ya mwaka mzima mtoto wa Shilole katika shule anayosoma, huku mpenzi wake Vanessa akijitolea kuwalipia Hoteli ya Nyota tano ya kilimanjaro, Shilole na mumewe Uchebe.


Msanii Shilole ambaye pia ni muigizaji wa filamu hapa nchini, amejikita kwenye ujasiriamali ambapo kwa sasa anamiliki mghahawa pamoja na bidhaa ya ‘shishi chili’.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527