JIPU LA AIRTEL,TTCL LAIVA..RIPOTI YA KAMATI YA UCHUNGUZI YATUA KWA JPM


Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amewasilisha kwa Rais John Magufuli taarifa ya kamati aliyoiunda kuchunguza umiliki wa kampuni ya simu Airtel na kueleza jinsi Serikali ilivyoingizwa mkenge.

Taarifa hiyo imewasilishwa  baada ya Rais Magufuli kutoa agizo la kufanyika hivyo Desemba 20 mwaka jana.

Baada ya kuwasilisha taarifa hiyo, Dk Mpango alisema Serikali imejiridhisha kuwa ubinafsishaji wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kwenda Celtel, baadaye kuhamishiwa Zain na sasa Airtel ulifanyika kwa ukiukwaji mkubwa wa sheria, kanuni na taratibu.

Kufuatia ukiukwaji huo Dk Mpango amesema Serikali inayomiliki asilimia 40 ya hisa za kampuni ya Airtel imeamua kufanya mazungumzo na kampuni ya Airtel inayomiliki asilimia 60 ya hisa ili nchi iweze kupata haki yake.

“Lakini niwaambie Watanzania yale ambayo tumeyaona ni machafu sana, ni mambo ya hovyo kabisa, nchi yetu kwa kifupi tuliingizwa mkenge, ni fedha nyingi zimepotea kwa hiyo sisi katika majadiliano haya lengo letu litakuwa ni kuhakikisha Watanzania wanapata haki yao,” alisema Dk Mpango.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527