WEZI WACHIMBA HANDAKI NA KUIBA MAMILIONI YA FEDHA BENKI KENYA

Maafisa wa polisi wanachunguza wizi wa shilingi milioni 50 uliofanyika katika tawi moja la benki ya KCB mjini Thika nchini Kenya.

Kufuatia kisa hicho kamanda wa polisi katika kaunti ya Kiambu Adiel Nyange amesema kuwa watu watatu wamekamatwa.

Kulingana na polisi hao, majambazi hao waliingia katika chumba cha kuhifadhi fedha cha benki hiyo kupitia handaki walilochimba chini ya ardhi na kuiba fedha hizo ambazo zilikuwa zimehifadhiwa ndani ya chumba hicho.

Wanaaminika kukata masanduku mawili ya kuhifadhia fedha hizo kwa kutumia mwako wa moto.

Polisi wanasema kuwa meneja wa benki hiyo aligundua kwamba benki hiyo imeibiwa muda wa saa mbili alfajiri wakati alipofungua chumba hicho cha kuhifadhia fedha.

''Majambazi hao lazima walikuwa na mtu anayefanya kazi katika benki hiyo aliyewaongoza hadi pale masunduku hayo yalipokuwa. Uchunguzi unaendelea'' , alisema naibu wa kamanda wa polisi Bernard Ayoo.
Chanzo-BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527