MECHI YA SIMBA, LIPULI YARUDISHWA UWANJA WA UHURU, YANGA ,PRISONS YABAKI CHAMAZI

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Lipuli iliyopangwa kuchezwa Jumapili, Novemba 26, 2017 kwenye Uwanja wa Azam Complex sasa itafanyika kwenye Uwanja wa Uhuru.

Awali mechi hiyo ilihamishiwa Azam Complex baada ya wamiliki wa Uwanja wa Uhuru kueleza kuwa utakuwa na matumizi mengine Novemba 26, 2017. Hata hivyo, Novemba 22, 2017 Bodi ya Ligi Kuu ilipokea barua kutoka kwa Mmiliki wa Uwanja wa Uhuru ikieleza kuwa uwanja wake sasa uko wazi kuwa mwenyeji wa mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 10 jioni.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527