WATOTO WATATU WAFARIKI KWA KULIPUKIWA BOMU ARUSHA..WALIDHANI NI MPIRA

Watoto watatu waliokuwa wakichunga ng'ombe katika Kijiji cha Nafco kilichopo Kata ya Loksale wilayani Monduli mkoani Arusha wamefariki dunia baada ya kulipukiwa na bomu walilolichezea wakidhani ni mpira.


Tukio hilo linadaiwa kutokea Ijumaa jioni ambapo Mwenyekiti wa kijiji hicho, Julius Mhale amesema watoto hao wanatarajiwa kuzikwa Jumatatu Septemba 18 
Mwenyekiti huyo amesema kuwa eneo ambalo bomu lililipuka hutumiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa mazoezi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa rasmi hapo baadae.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527