ASKARI POLISI AUA MKE KWA RISASI KISHA NAYE KUJIUA

Askari Polisi Stephen Mungai Kinuthia wa jimbo la Nakuru nchini Kenya, amemuuwa mkewe kwa kumpiga risasi kichwani na kisha kujiua mwenyewe mbele ya mtoto wao ambaye alishuhudia tukio zima.

Kinuthia ambaye alikuwa skari polisi wa kituo cha Molo, amempiga risasi mpenzi wake huyo mara tatu kwa kutumia bunduki ya AK47 wakiwa nyumbani kwao.

Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni mlinzi wa eneo hilo amesema walisikia kelele za watu wakilumbana, na walipokuwa wakikimbilia kujua kulikoni walisikia milio ya risasi na kisha kukawa na ukimya.

Majirani wa eneo hilo wamesema walisikia kelele za mtoto akilia kwa sauti huku akisema baba anamuuwa mama.

OCPD wa Nakuru Joshua Omukatta amesema wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo, huku miili ya marehemu wote ikiwa imepelekwa katika hospitali ya serikali ya Nakuru.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527