Tanzia : MSANII DOGO MFAUME ALIYEIMBA 'KAZI YANGU YA DUKANI' AMEFARIKI DUNIA



Msanii Dogo Mfaume Enzi za uhai wake



Msanii wa muziki wa bongo fleva, Dogo Mfaume ambaye aliwahi kutamba na nyimbo kama 'Kazi Yangu Ya Dukani' amefariki dunia leo 

Dogo Mfaume ambaye alitumbukia kwenye janga la madawa ya kulevya na baadaye kuanza kupata matibabu ya kuondokana na matumizi ya madawa hayo kupitia kituo cha Pilli Missana Foundation kilichopo Kigamboni.

Akiongea na EATV Pili Missana ambaye ni Mkurugenzi wa kituo hicho amethibitisha kufariki kwa msanii huyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527