DC SHINYANGA APONGEZA WANANCHI KUJENGA KITUO CHA POLISI ISELAMAGAZI,ANGALIA HAPA AKITEMBELEA JENGO LA POLISI

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro (pichani) amepongeza wananchi wa tarafa ya Nindo wilaya ya Shinyanga kwa kujenga kituo cha Polisi kata ya Iselamagazi ili kukabiliana na uharifu ambao umekithiri eneo hilo ukiwamo wa kuvamia watumishi wa serikali hasa walimu kisha kuwapora mali na kuwajeruhi kuwa katakata mapanga. Picha zote na Marco Maduhu Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikagua jengo la kituo cha Polisi kata ya Iselamagazi ambalo limejengwa kwa nguvu za wananchi wakishirikiana na mbunge wao wa Solwa Ahmed Salimu
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro  akitoa maelekezo kwa  watendaji wa kata,vijiji,vitongoji,viongozi wa Sungusungu na Madiwani wa halmashauri hiyo ya wilaya ya Shinyanga juu ya kutumia jengo hilo kikamilifu kutoa taarifa ya waharifu na kuchukuliwa hatua kali za kisheria
Ukaguzi wa jengo ukiendelea
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akishukuru wananchi kuhusu  ujenzi wa jengo hilo ambalo limejengwa kwa haraka ambapo ujenzi ulianza  Januari 12,2017 na limegharimu shilingi milioni 13.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro baada ya kumaliza kukagua jengo hilo la kituo cha polisi. Matiro aliwaahidi kuwaezekea paa ili lianze kufanya kazi haraka na kumaliza matukio ya uharifu kwenye tarafa hiyo ya Nindo na kudumisha amani kwa wananchi wote wakiwemo watumishi wa serikali.
Mkuu wa wilaya Josephine Matiro akiteta jambo na viongozi wa serikali pamoja na baadhi ya madiwani wa halmashauri kabla ya kuingia kwenye mkutano wa viongozi wa Sungusungu na watendaji wa vijiji,kata na vitongoji kujadili ajenda mbili za ulinzi na usalama pamoja na kuunda ushirika wa vyama vya kuuza mazao ili kuinua wakulima kiuchumi sambamba na kuhifadhi chakula cha akiba ili kukabiliana na janga la njaa hapo baadae.
Mkuu wa wilaya Josephine Matiro akizungumza na viongozi wa Sungusungu,baadhi ya watendaji wa kata ,vijiji,vitongoji na Madiwani wa halmashauri hiyo juu ya kudhibiti uhalifu kwenye tarafa hiyo ya Nindo pamoja na kuwafichua wahalifu ambao huhatarisha hali ya amani. 
Wajumbe wakisikiliza maagizo ya mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro kuhusu namna ya kudumisha amani na kutunza chakula cha akiba na kutokubali kulanguliwa mazao yao mashambani na wafanyabiashara na kuwafanya kuendelea kuwa maskini. 
Ofisa Tarafa ya Nindo Budugu Kasuka akitoa taarifa ya masikitiko kwa mkuu wa wilaya juu ya baadhi ya wananchi ambapo wamekuwa wakivamia watumishi wa serikali hasa walimu kwa kupora mali zao na kisha kuwa kata kata mapanga hali ambayo iliyowagusa wananchi wengi na kuamua kuchangisha pesa ili kujenga kituo cha polisi ambacho kitasaidia kudhibiti waharifu kwenye tarafa hiyo na kubainisha kuwa kituo hicho kitakuwa kimekamilika mwezi Juni 30 mwaka huu. 
Kikao kikiendelea huku wajumbe hao wakilitupia lawana jeshi la polisi kuwa pale wanapopelekewa waharifu hususani wale wanaotuhumiwa kukata mapanga walimu ambapo wao wamekuwa wakiwapatia dhamana na kisha kurudi mitaani kuanza kuwatambia na pia kuendeleza uharifu kama kawaida na hivyo kukata tamaa na kuogopa kutoa tena taarifa polisi licha ya kuwajua watu wote wanaofanya vitendo hivyo. 
Hapa wajumbe wakisikiliza majibu kutoka kwa kaimu kamanda wa jeshi la polisi wilaya Shadrack Zambi ambaye hayupo pichani kwa kufafaunua kuwa kila mtu ana haki ya kupewa dhamana, huku akibainisha watuhumiwa wote waliowakamata na kuwapeleka kwao kesi zao zinaendelea kusikilizwa mahakamani na endapo wakibainika kukutwa na makosa hayo watachukuliwa hatua za kisheria na pia kuwasisitiza wasichoke kutoa taarifa za waharifu ,huku akiwapongeza kwa ujenzi wa kituo hicho cha polisi ambacho kitasaidia kuongeza idadi ya askari wengi na hatimaye kufanikiwa kukomesha uharifu kwenye tarafa hiyo ya Nindo
Picha zote na Marco Maduhu Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527