RAIS MAGUFULI AWANYEMELEA WATUMISHI SERIKALINI WENYE VYETI FEKI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,John Pombe Joseph Magufuli,amejinasibu kutenda haki mara atapopata ripoti ya watumishi wa Serikali,waliogushi vyeti.

Kuna madai ya wafanyakazi wa Serikali zaidi ya elfu tisa kutumia vyeti vya kufoji,ambapo sasa Rais Magufuli, amefunguka kwa kusema sasa anasubiri ripoti ya wahusika hao ili aitendee kazi.


Rais Magufuli amesema hayo, wakati akizindua majengo ya Hostel za Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM),kwa kudai kumekuwa na changamoto kubwa katika kila sekta hivyo sasa anasubiri hiyo ripoti ili aweze kuifanyika kazi na kutenda haki katika jambo hilo.


Anasema;"Naisubiri ripoti ya wafanyakazi wa Serikali zaidi ya elfu tisa ambao wana vyeti vya kufoji ili niifanyie kazi." 


Mbali na hilo Rais Magufuli ameitaka Taasisi ya TCU kuacha kuwapangia wanafunzi vyuo bali wanafunzi wanapaswa kuwa huru kuchagua aina ya vyuo ambavyo wao wanataka kwenda kusoma.


Amefafanua kwa kusema kufanya hivyo itatoa nafasi kila chuo kuwa na wanafunzi wa kutosha huku wanafunzi pia wakienda kusoma sehemu ambazo wao wanahitaji kwenda kusoma na si kuwapangia.


"Mtu amefaulu ana sifa zake anataka kuja kusoma Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam afaidi mabweni ya Magufuli analazimishwa kupelekwa kwenye ka chuo ambako wala hakana jina hata ukitafuta kwenye mtandao hakaonekani, akasome pale wakati hawana hata mabweni na saa zingine hata walimu hawana, tunawatesa watoto hawa,”


“… na saa zingine wakuu wa vyuo vile wamekuwa na tabia ya kwenda kwenye uongozi wa TCU ingawa sina ushahidi wapangiwe idadi wa wanafunzi wanaowataka kwenye vyuo hivyo,”




“….sifahamu wanapangiwa kwa rushwa,lakini wapo pia kuna ushahidi na baadhi ya viongozi wa vyuo fulani fulani waliofunga safari kwenda TCU kwa ajili ya kuomba wapangiwe wanafunzi au kutoa shukrani, au hata kwenda kuwasalimu tu" alisema Rais Magufuli.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527