KUHUSU AJALI YA BASI KUGONGA TRENI KISHA KUJEUHI NA KUUA

Mtu mmoja amefariki dunia baada ya kutokea ajali ya basi la abiria/daladala (T 435 DGG) kutoka Gongo la Mboto kwenda Mnazi Mmoja kuigonga treni ya Pugu leo Aprili 19, 2017 saa 11 alfajiri katika makutano ya reli na barabara ya Nkurumah jijini Dar es Salaam.

Majeruhi wa ajali ni 23 , wanane wapo hospitali ya Amana na waliobakia 15 wapo Hospitali ya Taifa Muhimbili MOI watatu kati yao ni mahututi. Taarifa zaidi itatolewa kuhusu ajali hiyo.

Hata hivyo treni ya Pugu inaendelea na huduma zake kwa kufuata ratiba.

Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL

Nd. Focus Sahani,
Dar es Salaam,
Aprili 19, 2017.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527