MWANAMKE APIGWA RISASI BAADA KUGONGA POLISI

Mwanamke ajaribu kugonga polisi akitumia gari Washington

Polisi mjini Washington nchini Marekani, wamemfyatulia risasi mwanamke mmoja aliyekuwa ndani ya gari, baada ya yeye kugonga gari la polisi karibu na bunge la Marekani na baadaye kujaribu kuwagonga maafisa kadha wa polisi.

Mwanamke huyo hakupigwa risasi, kwa mujihu wa msemaji wa polisi mjini Washington.

Alikamatwa na kisa hicho kikasababisha kufungwa kwa moja ya majengo ya bunge.

Kisa hicho kinajiri baada ya kushuhudiwa mashambulizi kadha ya kugonga kwa magari miji ya London na Brussels,

Msemaji wa polisi Eva Malecki, amesema kuwa mshukiwa ni mwanamke na kisa hicho ni cha uhalifu.Polisi wakiweka ulinzi katika bunge la Marekani

Kisa hicho kilitokea wakati maafisa waligundua dereva ambaye alikuwa akiendesha gari kwa njia isiyo ya kawaida na kutaka kumsimamisha.

Dereva huyo kisha akageuza gari kwa haraka na nusura awagonge polisi.

Sababaua ya kisa hicho haijulikani na mwanamke huyo hajatambuliwa.

Vikao vya bunge vinaendelea kama kawaida na watalii wameruhusiwa kurudi eneo hilo.
Via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527