DC KAHAMA APIGA MARUFUKU WALIMU WAKUU KUZUIA KUANDIKISHA WANAFUNZI WASIO NA VYETI VYA KUZALIWA


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Fadhili Nkurlu amewapiga marufuku walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari kuzuia kuandikisha wanafunzi wa kidato cha kwanza na darasa la kwanza hadi wawe na vyeti vya kuzaliwa.




Nkurlu alitoa agizo hilo baada ya baadhi ya wazazi na wanafunzi kufika ofisini kwake kusaka vyeti na wengine kulalamika kitendo cha walimu kuwazuia kuanza kidato cha kwanza.


“Ni marufuku kwa mwalimu yeyote au kiongozi kuzuia wanafunzi kuandikisha kwa madai ya cheti cha kuzaliwa kama wanataka kujiridhisha wapate barua kutoka kwa mwenyekiti wa kitongoji au watendaji wa kijiji na siyo cheti hicho,” alisema Nkurlu.


Mmoja wa maofisa elimu kutoka Halmashauri ya Mji wa Kahama, Aruko Lukolela alisema agizo la mkuu wa wilaya litatekelezwa mara moja.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527