Makubwa Haya!! MBWA ACHOMWA MSUMARI KICHWANI KISHA KUZIKWA AKIWA HAI



Mbwa mmoja amepatikana amezikwa akiwa hai huku msumari ukiwa umedungwa kichwani mwake katika eneo la Teesside katika kile shirika linalokabiliana na unyanyasaji wa wanyama nchini Uingereza RSPCA linasema ni kitendo cha ukatili.

Wanandoa wawili waliokuwa wakitembea katika eneo la Kirkleatham Wood ,walisikia kilio cha kitu kilichokuwa kikilia kwa uchungu na kumpata mbwa huyo ambaye tayari alikuwa amezikwa.

Alikimbizwa kwa daktari wa wanyama lakini majeraha yake mabaya yalimlazimu mtabibu huyo kumuua.

Shirika hilo la wanyama linasema kuwa zaidi ya mtu mmoja alihusika katika kitendo hicho.

Inspekta Nick Jones alisema: katika kipindi cha miaka kumi ambacho nimefanyia kazi RSPCA,sijawahi kuona kitu cha kuogofya na ukatili mkubwa kama huu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527