Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MTOTO ALIYEBAKWA NA KUTOBOLEWA MACHO SHINYANGA AZIKWA ,ANGALIA PICHA YAKE HAPA

Happiness Kashinje enzi za uhai wake

Mazishi ya mwili wa mtoto Happiness Kashinje(9) aliyeuawa kikatili kwa kubakwa kisha kutobolewa macho na watu wasiofahamika kisha mwili wake kutupwa kichakani katika kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga yamefanyika leo mchana katika makaburi ya familia nyumbani kwa babu yake katika kijiji cha Negezi kata ya Mwawaza katika manispaa ya Shinyanga.

Mtoto Happinss aliyekuwa anasoma darasa la tatu katika shule ya Msingi Negezi iliyopo kata ya Mwawaza katika manispaa ya Shinyanga alikutwa ameuawa kwa kubakwa kisha kutobolewa macho juzi saa saba mchana katika kitongoji cha Kashampa kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi ndani ya manispaa ya Shinyanga

Mazishi hayo yamehudhuriwa na walimu na wanafunzi wa shule  aliyokuwa anasaoma mtoto huyo,wakazi wa eneo hilo pamoja na maeneo ya jirani,wadau wa haki za watoto,waandishi wa habari,mkuu wa intelijensia mkoa wa Shinyanga,viongozi wa dini na siasa wakiongozwa na naibu meya wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila.


Akizungumza wakati wa mazishi hayo yaliyohudhuriwa pia na Malunde1 blog naibu meya wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila amelaani kitendo cha kinyama alichofanyiwa mtoto huyo huku akiitaka jamii kushirikiana na jeshi la polisi katika kuwafichua wahusika wa mauaji hayo.

Naye mkuu wa Intelijensia mkoa wa Shinyanga Bundala Maige amesema suala la ulinzi kwa watoto ni la jamii nzima na kwamba wahalifu wako ndani ya jamii hivyo kuitaka jamii kuwafichua wahalifu hao ili kukomesha vitendo vya ukatili vinavyoendelea mkoani Shinyanga.

Kwa upande wake mwinjilisti  Emmanuel Donald Kaswalala aliyeendesha ibada ya mazishi alilaani vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watotot huku akiiomba jamii kumrudia mwenyezi mungu kwa kuondokana na matendo mabaya.

Na Kadama Malunde-Shinyanga

ANGALIA PICHA ZOTE ZA MAZISHI YA MTOTO HAPPINESS HAPA

TAFADHALI BOFYA HAPA U LIKE PAGE YETU TUKUTUMIE "HABARI" MOJA KWA MOJA KILA ZINAPOTOKEA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com