Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KAMATI YA FEDHA,UTAWALA NA MIPANGO YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KISHAPU



Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe. Enock Reuben Bundala na Diwani wa Kata ya Masanga (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Emmanuel Johnson Matinyi (kushoto) kwenye ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo wilayani humo Januari 14-15,2025


Na Sumai Salum-Kishapu


Kamati ya Kudumu ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo yenye zaidi ya Tsh. Bil. 1.2.


Ziara hiyo iliyohusisha baadhi ya Madiwani na Menejimenti imefanyika mnamo Januari,14-15, 2026 Kata ya Kishapu,Lagana,Talaga,Maganzo,Songwa,Mondo na Sekebugoro huku ikikagua jumla ya miradi tisa.


Tazama picha za miradi mbalimbali


Ujenzi wa Madarasa 2 ya Awali na Matundu 6 ya Choo – Shule ya Msingi Isoso wenye thamani ya Tsh 71,800,000 chanzo cha fedha ni mradi wa Boost

Ujenzi wa Vyumba 6 vya Madarasa, Jengo la Utawala na Vyoo – Shule ya Sekondari Isoso wenye thamani ya Tsh 342,900,000 chanzo cha fedha ni mradi wa Boost


Ujenzi wa Kituo cha Afya Lagana (OPD na Maabara) wenye thamani ya Tsh 250,000,000 chanzo cha fedha ni kutoka serikali kuu

Ujenzi wa Vyumba 2 vya Madarasa na Matundu 6 ya Choo – Shule ya Msingi Nhobola wenye thamani ya Tsh 66,200,000 chanzo cha fedha ni mradi wa BoostUjenzi wa Vizimba 200 – Soko la Maganzo mradi unaotekelezwa kwa fedha za CSR ya Mgodi wa Almas Mwadui WDL wenye thamani ya Tsh 260,000,000


Ujenzi wa Matundu 5 ya Choo –soko la Maganzo fedha za CSR kutoka Mgodi wa Almas Mwadui WDL wenye thamani ya Tsh 20,000,000
Ujenzi wa Ofisi ya Kijiji cha Songwa kwa fedha za CSR kutoka Mgodi wa Almas Mwadui ( WDL) wenye thamani ya Tsh 47,000,000
Ujenzi wa Vyumba 2 vya Madarasa – Shule ya Msingi Buchambi fedha za CSR wenye thamani ya Tsh 48,000,000


Ujenzi wa Zahanati ya Seke Ididi wenye thamani ya Tsh 101,989,971 chanzo cha fedha kikiwa ni CSR kutoka kampuni ya ujenzi ya CCECC

















































Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com