BHUDAGALA AKATISHA SHOW LWAMUGASA GEITA MAELFU WAKIKANYAGANA UWANJANI ...SHUHUDIA HAPA

Msanii maarufu wa Nyimbo za asili Bhudagala Mwanamalonja kutoka Serengeti mkoa wa Mara leo Jumanne Mei Mosi 2018 amelazimika kumaliza show yake kabla ya wakati kutokana na Maelfu ya Mashabiki zake kufurika katika Uwanja wa Mpira wa katika kijiji cha Lwamugasa kata Lwamugasa wilaya ya Geita mkoani Geita.

Show ilianza majira ya saa saba mchana lakini kutokana na mashabiki kufurika uwanjani kwa kiwango ambacho hakikutarajiwa,Bhudagala akalazimika kukatisha show saa kumi jioni kwa ajili ya usalama wa watu waliohudhuria show hiyo ya historia kwa kila mmoja alikuwa ana shauku ya kujionea show hiyo hivyo kusababisha mkanyagano uwanjani.

Nimekuwekea Video na Picha hapa chini jinsi hali ilivyokuwa
VIDEO


Mashabiki wa Bhudagala wakiwa uwanjani
Bhudagala akiwa juu ya spika walau mashabiki wamuone tu
Bhudagala akiwa juu ya spika
Mashabiki wa Bhudagala wakiwa uwanjani






Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527