WANAJESHI WALISHWA DAMU NA NYAMA YA NYOKA


ASKARI wa Jeshi la Majini la Marekani, wamekuwa wakipewa mafunzo ya uuaji nyoka aina ya Cobra na wakufunzi wa majini kutoka nchini Thailand, kabla ya kutakiwa kunywa damu ya nyoka hao, nyama yao na hata kula nyama ya kuku.

Wakufunzi hao pia waliwaonyesha askari hao mende wanaoweza kuwala wawapo msituni, lakini pia jinsi ya kuwawezesha kuwa salama.

Zoezi hilo la uuaji nyoka hao lililopewa jina la Cobra Gold, ni miongoni mwa mipango ya jeshi hilo la Marekani ambalo limejikuta likiwavuta watu wapatao 13,180 kutoka nchi mbalimbali kama Thailand, Marekani, Singapore, Japan, Jamhuri ya Korea, Indonesia na Malaysia.

Mafunzo hayo yamekuwa yakiambatana na kusaidia shughuli mashambani na miradi mbalimbali ya kibinadamu na ya kiraia inayoongeza kiwango cha maisha kwa watu wa Thai na jirani zao.

Miongoni mwa shughuli hizo ni mafunzo ya mapambano dhidi ya wapiganaji, operesheni ya kutafuta na kukamata silaha na wavamizi bila kutumia nguvu .

Kila mwaka kumekuwa kukiendeshwa mafunzo hayo ya kimataifa kwenye pwani ya Hat Yao, mashariki mwa Thailand, kwa kutumia magari ya mashambulizi.

Zoezi hilo la kijeshi la wiki mbili, huu ni mwaka wake wa 31, pia likitoa nafasi kwa majeshi ya Marekani kuendeleza uhusiano wa karibu na wanajeshi wa Asia.

Naibu Mkuu wa mpango huo katika Ubalozi wa Marekani nchini Bangkok, Judith Beth Cefkin anasema: “Sisi tunajivunia uhusiano na ushirikiano wetu na Thailand, lakini pia ushirikiano wetu na Asia.

“Uhusiano huu wenye msingi wa urafiki, malengo ya pamoja na kuheshimiana hufanya Cobra Gold kuwa zoezi muhimu na mahiri leo hii.”

Mwaka jana, Marekani ilitangaza mkakati wa kujiunga tena na Asia ya Kusini Mashariki ambayo ilikuwa ni pamoja na kudumisha misingi mikubwa ya kijeshi nchini Japan na Korea ya Kusini na kuongezeka kwa idadi ya majeshi katika ukanda huo.

Admiral wa nyuma Scott Jones, mkuu wa Jeshi la Amphibious Force 7, aliiambia navaltoday.com: “Mazoezi kama Cobra Gold ni muhimu kujenga na kudumisha mahusiano na washirika wa nje katika mkoa wa Asia na Pasifiki.

“Cobra Gold ya mafunzo ya wafanyakazi wa majini inasaidia ushirika wetu wa kukabiliana na mgogoro katika shughuli mbalimbali.”

Inayofuata Operesheni Bold Alligator, ambayo iliona wafanyakazi wa huduma 20,000 kutoka Marekani, Uingereza, Ufaransa, Canada, Hispania, Italia, Uholanzi, New Zealand na Australia vilima vilivyokuwa viko katika North Carolina na Virginia kama sehemu ya zoezi kubwa la kimataifa miaka kumi.

Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Force 7th Fleet cha Jeshi la Marekani, Scott Jones, aliuambia mtandao wa navaltoday.com: “Mazoezi kama la Cobra Gold ni muhimu ili kujenga na kudumisha uhusiano mzuri na rafiki zetu wa ukanda wa Asia na Pasifiki.

“Mafunzo ya Cobra Gold yanasapoti uwezo wetu wa pamoja katika kukabiliana na majanga mbalimbali katika maeneo yetu.”

Katika operesheni iliyofuata ya Bold Alligator, ambayo ilihusisha watu 20,000 kutoka Marekani, Uingereza, Ufaransa Canada, Hispania, Italia, Uholanzi, New Zealand na Australia, wiki iliyopita iliweka kambi katika fukwe za North Carolina na Virginia kama sehemu ya tukio kubwa kuwahi kutokea ndani ya muongo la mafunzo hayo.

Chanzo- Mtanzania

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527