KAULI YA DIAMOND,NANDY BAADA YA KUTOKA TCRA SAKATA LA PICHA CHAFU MTANDAONI

Wasanii Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Faustina Charles ‘Nandy’ wamehojiwa kwa saa mbili na Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA).



Wakizungumza mara baada ya kumaliza mahojiano hayo yaliyofanyika leo Aprili 19, wasanii hao wamesema wamejifunza mengi kuhusiana na masuala ya mitandao.

Diamond amesema: “Ujana ni maji ya moto tumeelimishwa, hatutarudia tena, nitakuwa balozi kwa vijana wenzangu kuhusu masuala ya mitandao.”

Nandy amesema: “Nisameheni kwa yaliyotokea. Hapa TCRA nimepata somo kuhusu mitandao, tukio lile halitajirudia tena.”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527