Picha & Video : MSANII MAARUFU BHUDAGALA AKITAMBULISHA NYIMBO 6 MPYA 'ALBAMU YA BHUHABHI' SHINYANGA...NI BALAA!!

Msanii maarufu wa nyimbo za asili Bhudagala Mwanamalonja kutoka Serengeti mkoani Mara Jumanne Aprili 3,2018 ametambulisha rasmi albamu yake mpya aliyoipa jina la Bhuhabhi 'Umaskini'.

Bhudagala ametambulisha albamu hiyo yenye nyimbo sita katika uwanja wa SHIRECU vilivyopo kwenye mji wa Mhunze wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga. 

Miongoni mwa nyimbo zilizopo katika albamu hiyo ni Mbalu,Mali ya baba,Tulebhalyo,Kabhula,Bhokoo na Bhuhabhi inayobeba jina la albamu.

Akizungumza na Malunde1 blog ambayo ni mdau mkubwa wa nyimbo za asili,Bhudagala amesema nyimbo hizo zenye ujumbe mzito ni zawadi kwa mashabiki wake na kuwaomba kuzipokea.

Mwandishi wetu Kadama Malunde ametuletea video na picha za matukio yote

Msikilize hapa akizungumzia nyimbo mpya.

SHUHUDIA HAPA SHOW YA BHUDAGALA AKITAMBULISHA ALBAMU MPYA YA BHUHABI


Msanii maarufu wa nyimbo za asili Bhudagala Mwanamalonja akitambulisha rasmi albamu yake mpya ya Bhuhabhi leo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Bhudagala Mwanamalonja akiimba wimbo wa Bhuhabhi
Wanenguaji wa Bhudagala Mwanamalonja wakionesha mbwembwe zao
Wanenguaji wa Bhudagala wakicheza
Wanenguaji wa Bhudagala wakionesha vipaji vyao vya kucheza
Burudani inaendelea
Bhuhabi nomaaa!!

Wananchi wakishuhudia burudani

Burudani inaendelea..
Hatariiii
Bhudagala pia ana kundi la vijana wa sarakasi...hapa wanafanya yao


Kamgeuza kiti mwenzake..
Kuruka kwenye ringi mbili....

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527