Breaking : WATU NANE WAFARIKI AJALI YA BASI KUGONGANA NA NOAH MBEYA

WATU nane wamefariki dunia papo hapo na mmoja amejeruhiwa baada ya gari dogo aina ya Toyota Noah kugongana na basi katika eneo la Igodima nje kidogo ya Jiji la Mbeya. Kaimu Kamanda wa Polisi Mbeya, Mussa Taibu amethibitisha. 

Ajali hiyo imetokea leo Jumatatu Aprili 9, 2018 mchana ikihusisha Noah yenye namba za usajili T 649 DEA na basi la Igembesabo katika Barabara ya Chunya Mbeya huku chanzo cha ajali hiyo kikiwa hakijulikani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527