Breaking News: MMILIKI WA MABASI YA HBS NA SABENA AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI


Basi la HBS
Basi la Sabena

Mfanyabiashara anayefahamika kwa jina la Sultan Ahmed au maarufu Chapa mmiliki wa kampuni ya mabasi ya HBS na Sabena amejipiga risasi mdomoni na risasi kutokea nyuma kichwani 'kisogoni'. 


Tukio hilo limetokea leo Jumatano Aprili 11,2018 saa tatu asubuhi  ambapo mfanyabiashara huyo mwenye asili ya kiarabu ambaye ni  lakini pía ni mmiliki wa kituo kikubwa cha uuzaji wa mafuta ya petroli wilayani Sikonge amejipiga risasi akiwa nyumbani kwake huko wilayani Sikonge mkoani Tabora.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora SACP Wilbroad Mutafungwa amethibitisha tukio hilo na kwamba wanafanya uchunguzi juu ya mauaji hayo.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527