DIAMOND AANIKA MAHABA YAKE KWA WEMA SEPETU LIVE BILA CHENGA

Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz ameshindwa kujizuia baada ya mpenzi wake wa zamani na Malkia wa Bongo Movies, Wema Sepetu kutupia picha yake na kumtag akisema “I’m inlove with you there’s nothing dat I wouldn’t do, catch a grenade for you, as long as you want me to…” jambo lililomuibua Diamond na kuanika rasmi mahaba yake kwa Wema.



Hayo yamejiri ikiwa ni saa chache baada ya Wema kuposti kipande cha wimbo mpya wa Diamond aliyomshirikisha staa wa Marekani, Omario, ngoma inaitwa AFRICAN BEAUTY na kumfagilia kwa kazi nzuri aliyoifanya.



Kwa mujibu wa mashabiki wa mastaa hao, inaonekana wamesharudiana na sasa wanaanza kuanika uhusiano wao.


Hivi karibuni ameachana na mama watoto wake, Zari The Bossy Lady kwa kile kilichodaiwa sababu kuwa Diamond amezaa na mwanamitindo Hamisa Mobeto.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527