MSAIDIZI WA LISSU : MAHAKAMA SIYO SEHEMU YA MAJARIBIO..WATENDAJI WOTE WAIHESHIMU

Makamu wa Rais wa chama cha wanasheria Tanganyika (TLS), Wakili Godwin Ngwilimi amemtaka Jaji Mkuu wa Tanzania pamoja na watendaji wote wa sheria kuiheshimu mahakama kwani ni sehemu ambayo ukienda mwishowe haki inapatikana.

Akizungumza jana wakati alipokuwa kwenye maadhimisho ya wiki ya sheria ambapo ameonya mahakama zisitumike kuonea watu wengine huku akikazia kuwa mahakama haipaswi kuwa sehemu ya majaribio kwani siyo maabara.

"Msiruhusu hata mara moja kwani mnalindwa na Katiba. Msimamie hayo ili mahakama isiendelee kuonekana sehemu ya mchezo mchezo. Maisha ya jamii ni mapana kuliko migogoro au hata sheria. hivyo nadiriki usema kwamba siyo lazima maisha ya jamii ni sheria au ni lazima yaishe kisheria au mahakamani." Tusichukulie Mahakama kama jumba la kamari," Wakili Ngwilimi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527