KATAMBI ATAJA SABABU ZA KUHAMIA CCM


Aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Patrobas Katambi aliyehamia CCM Novemba, 2017 ametoa sababu sita za kukihama chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 2, 2018 jijini Dar es Salaam, Katambi amesema ameamua kueleza hayo baada ya kujipa muda wa kutafakari kwa kina.

Amesema sababu ya kwanza ni vyama vya upinzani ikiwamo Chadema kushindwa kujipambanua kama taasisi, badala yake kuwa kama cha mtu binafsi.

Katambi amesema sababu nyingine ni ukosefu wa maamuzi shirikishi, ukiukwaji wa katiba na misingi ya demokrasia, kutokuwa na mawasiliano na umoja na kukosa maadili kwa viongozi.

"Hali hii ya ukosefu wa maadili inasababisha matumizi mabaya ya mali za chama na sababu ya mwisho ni chama kukosa ajenda," amesema Katambi.

Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527